Sunday, October 25, 2009

LUTHERAN :Sasa ruksa ndoa za jinsia moja

Picha ya kanisa la kilutheri jijini Stockholm,Sweden.

Ukistaajabu ya Musa,utayaona ya Firauni

Kanisa la kilutheri nchini Sweden lenye waumini wengi zaidi nchini humo limekubali kubariki ndoa za wapenzi wa jinsia moja kuanzia mwezi ujao.

Asilimia 70 ya baraza kuu la kanisa hilo lilipigia kura kuunga mkono hatua hiyo. 

Serikali ya Sweden imepitisha sheria mpya kulinda wapenzi wa jinsia moja. Robo tatu ya raia wa Sweden ni waumini wa Lutheran, japo idadi ya wanaohudhuria ibada imepungua sana.

Kaziiiii kweli kweli?Sijui tutafika kweli?

Chanzo cha habari BBC.CO.UK/SWAHILI

12 comments:

Yasinta Ngonyani said...

MMMhhh! Kaka Edo ni kweli kaaazzii kwelikweli lakini tusikate tamaa

Mwanasosholojia said...

Pamoja na uhuru wa kujiamria mambo pasipo kuvunja sheria...hii sasa inaleta taabu kidogo...!

chib said...

Sielewi uelekeo wa dini hasa huko majuu uko wapi!
Nahisi waafrika karibu watabadili makanisa majina na kuyaita ya majina ya kiafrika.

EDWIN NDAKI said...

@Yasinta ndio maendeleo hayo

EDWIN NDAKI said...

@Chibi tunapoelekea panatisha

EDWIN NDAKI said...

Mwanasosholojia..ndio maendeleo na uhuru tunapoenda naogopa hata kufika

Candy1 said...

Mmh, mie sijui!

SIMON KITURURU said...

Sasa hivi tutafikia katika maswala ni WACHAWI ndio wanaoeleweka KIIMANI!

Dini bomba la kitu cha WENGI ndio maana kama nini yako uko pekee kuna watakao dai hiyo sio dini kwa kuwa haina SHEKHE.:-(

akyoo said...

saint simoni!

mkonowangu said...

Watu hatutaki kuukubali ukweli basi acha yatukute..adhabu ni moto wa milele....

EDWIN NDAKI said...

St Kitururu umenimaliza kabisa..haaahaaa

EDWIN NDAKI said...

@adamu kweli watu wameamua kufuata njia zao..

hapa pakuwa pagumu