Monday, June 23, 2014

BONGO FC (Finland) WAISAMBARATISHA NIGERIA 4- 2

Timu ya watanzania Bongo FC yenye maskani yake Finland.Picha baada ya pambano lake na timu ya Nigeria na kufanikiwa kuzoa ushindi mnene wa mabao 4-2.

Bongo FC miongoni mwa timu kongwe na kielelezo cha uwakilisha wa Tanzania kwenye ukanda wa nchi za 'scandnavia'.

Bongo FC imefanikiwa kuanza kampeni yake ya msimu wa majira ya kiangazi kwa kucheza michezo miwili.Mchezo wa kwanza waliifunga timu Ethiopia magoli  5-3 na mwishoni mwa juma kuifunga timu ya Nigeria 4-2.

Wafungaji wa magoli akiwa Mwita Chacha , Bakari Salehe, Tonny aka Diego Simeon..Hizi ni salaam kwa ndugu zetu wa Sweden Kilimanjaro FC...

Hongera Bongo FC

Tutafika tu