Friday, February 17, 2017

Leo nairejesha EDONDAKI.BLOGSPOT.COM baada ya mapumzika ya miaka miwili na nusu..NIPOKEENI





Pichani jana nikiwa mji mkuu wa Jamuhuri ya Czech, Prague.

Salaam kutoka Jamuhuri ya watu wa Czech. Nilianza kublog mwaka 2007 hadi 2014. Baadaye niliamua kupumzika kublog. Nilipendelea kutuma picha na habari fupi, ikiwa ni sehemu ya kutumia taaluma yangu ya habari niliyoipata chuo kikuu cha SAUT mwanza na Tampere,hapa Finland.

Baada ya mapumziko ya tangu Juni 2014, ikiwa ni miaka miwili na miezi saba, leo nimeamua kurejea kwenye hili 'libeneke' kama anavyoliita nguli wa blog ISSA MICHUZI .
Mengi yamejitokeza, blog nyingi zimezaliwa na kufa ktk kipindi hiki. Sisi tulipoanza ilikuwa lengo kuu ni kuhabarisha, kabla kuwa 'chanzo cha kipato'.

SASA NAREJEA TENA KWENYE HII MEDANI. TUTAFIKA TU

Kama ulivyo msemo mkuu wa hii blog TUTAFIKA TU.

Wasalaam 

Edo Ndaki
edondaki.blogspot.com

Prague, Czech.
17-02-2017

2 comments:

Yasinta Ngonyani said...

AFadhali uredi bwana maana wanablogg wengi wa miaka ile hawapo...Binafsi nakukaribisha na kukupokea kwa mikono miwili pia kwa furaha tele jirani yangu...kweli ni kipindi sasa ...habari za tangu mwaka juzi:-)

EDWIN NDAKI (EDO) said...

Asante sana dada Yasinta. hongera sana kwa kuweza kudumu na kwanguvu zote