Friday, May 30, 2014

WORLD VILLAGE FESTIVAL 2014-HELSINKI FINLAND

Baadhi ya watanzania waishi jiji la Helsinki Finland picha ya pamoja muda mfupi baada ya maandalizi ya banda la jumuiya ya watanzania na finland  (STS) kwenye maonyesho ya "World Village Festival'

Kutoka kulia Noeli Makumuli mjumbe wa bodi , msaani wa kimaitaifa wa Raggae kutoka Tanzania Jhikoman pamoja na Edo Ndaki Mwenyekiti wa Finland Tanzania Friendship society - STS

Picha huongea maneno zaidi ya elfu moja.Hakika banda la wawakilishi wa Tanzania lilifana na kutembelewa na wageni wengi.

Kutoka kulia bw Fidelis Tungaraza akitoa ufafanuzi kwa mgeni aliyetembelea banda huku bw Edward Mtafungwa na Noel Makumuli viongozi wa bodi ya STS wakiendelea kuhabarisha wageni mambo mbalimbali yahusuyo Tanzania.

Mark Mhekwa kati ya watanzania waliopata muda wa kutembelea banda la maonyesho la jumuiya ya watanzania na wafini.

Naam,Moudy alimletea binti yake kumnunulia vitabu pamoja na cd za kiswahili ili aweze kujifunza lugha ya baba.Safi sana.

"One loveeeeeeeeeee" kutoka kushoto msanii wa muziki wa Raggae kutoka Bagamoyo Tanzania Jhikoman, nguli Popo pamoja na makamu mwenyekiti wa jumuiya Ilona Tika.

'Karibu Tanzania' nilitembelea na mwanafunzi ninayesoma naye chuo kimoja .Hakuondoka hivi hivi alivutiwa na kitabu chetu cha 'KARIBU TANZANIA'

Wadau wa jiji la Helsinki..Hii picha naomba msaada wa caption :D