Wednesday, November 11, 2009

TANZANIGHT SHOW -Tampere Ufini


Menard Mponda ..tabasamu kuuuuubwa baada ya kushuhudia TANZANIGHT SHOW


Huyu "braza" alipiga ngoma balaa..Show ilikuwa kali

Kama kawaida msanii wa Bongo Flava Benjamini wa mambo Jambo akikamua

SANAA SANA kundi kutoka Tanzania lilifanya show kali na kuacha watu wakipagawa.

Pamoja tunawakilisha

Tuesday, November 10, 2009

TANZANIA NIGHT TAMPERE FINLAND

Ras Jhikoman akipagawaisha mashabiki wa Finland kwa Raggae nzito yenye vionjo ya "ala za kitanzania na magharibi"

Msanii Mashimba aliweza kukong'a vilivyo nyoyo za mashabiki baada ya kuwapa vionjo mbalimbali.

Msanii wa Bongo Flava Dudu baya akiwa akisindikizwa jukwaani na wasanii wa kundi la SANAA SANA

Benjamin wa Mambo jambo akiwawasikilisha kwa hisia kali!..mambo ya "embe dodo"

Mika Mwamba "producer" akiwasha moto kwenye ukumbi wa Klubi Tampere .



Mwisho wa juma ulimalizika kwa burudani kubwa ya kukatwa na Mundu.Vikundi vya burudani kutoka Tanzania na wasanii waliweza kutoa burudani kali ndani yajiji la Tampere..

Habari zaidi na picha naziweka muda si mrefu..Cheki kwanza hizo chache

Wednesday, October 28, 2009

DA SUBI kahamia WWW.WAVUTI.COM


Katika kupita pita hapa na pale.Nimegundua Da Subi ambaye alikuwa anaishi na kupatikana kupitia www.nukta77.blogspot.com

Sasa amehamia kwenye makazi mapya ambayo ni www.wavuti.com

Namtakia mafanikio katika makao mapya

Tutafika tu


Sunday, October 25, 2009

LUTHERAN :Sasa ruksa ndoa za jinsia moja

Picha ya kanisa la kilutheri jijini Stockholm,Sweden.

Ukistaajabu ya Musa,utayaona ya Firauni

Kanisa la kilutheri nchini Sweden lenye waumini wengi zaidi nchini humo limekubali kubariki ndoa za wapenzi wa jinsia moja kuanzia mwezi ujao.

Asilimia 70 ya baraza kuu la kanisa hilo lilipigia kura kuunga mkono hatua hiyo. 

Serikali ya Sweden imepitisha sheria mpya kulinda wapenzi wa jinsia moja. Robo tatu ya raia wa Sweden ni waumini wa Lutheran, japo idadi ya wanaohudhuria ibada imepungua sana.

Kaziiiii kweli kweli?Sijui tutafika kweli?

Chanzo cha habari BBC.CO.UK/SWAHILI

Hongera EMMA kwa KUFUNGA NDOA

Wakili Emmanuel Tamira Makene akiwa na mke wake bi Sarah Twilumba muda mfupi baada yakufunga pingu za maisha.
Picha kutoka blog ya Issa Michuzi 

Leo wakati nikitafuta nini cha kuandika ghafla nakutana na picha ya school mate wangu akimeremeta.

Bwana harusi ambaye kwa sasa anamiliki kampuni yake binafsi ya uwakili ya Kings Law Chamber.Kabla ya hapo alikuwa wakili wa magazeti ya serikali ya Tanzania Standard news paper.

Kwa kifupi huyu mheshimiwa ni miongoni mwa walinitupokea seminarini tukitafuta wito wa upadre,yeye akiwa kidato cha tatu mimi ndio "nyoya",bazoka, fomu wani.

Kwa mfumo wa seminari mara nyingi kidato cha tatu ndio wanakuwa wapo karibu sana na kidato cha kwanza kuliko kidato cha pili.

Kwa wale wanajua maisha ya shule nyingi za bweni za miaka hiyo kidato cha pili wao ndio "Military police"MP wa shule.

Bwana harusi alikuwa katibu wetu wa Debate club. 

Binafsi nimefurahi na ninafurahi kuona watu ninao wafahamu wakiendelea kupiga hatua flani flani katika maisha.Namtakia kila la kheri katika maisha ya ndoa.

Unakumbuka nini kuhusu maisha ya shule?



Friday, October 23, 2009

HAPPY BIRTHDAY RAIS PAUL KAGAME

Nelson Mandela akiwa na Rais wa Rwanda Paul Kagame.
(Picha na Denis Farell)

Leo Oktoba 23 ni "birthday" ya rais wa Rwanda Paul Kagame.Alizaliwa mji Gitarama,Rwanda  october 23,1957.

Akiwa na umri wa miaka(2) alikimbia yeye na familia yao pamoja na familia zingine za kabila la watutsi Uganda baada ya mauji yalioendeshwa na serikali ya wahutu nchini Rwanda.

Kwa zaidi ya miaka 30 aliishi ukimbizini nje ya nchi yake.Kwa msaada wa rafiki yake(Rais Yoweri Museveni) aliweza kuanzisha harakati za Rwandese Patriotic Front 

April 6,1994 ndege iliyokuwa imembeba rais wa Rwanda Juvenal Hybarimana na rais wa burundi  Cyprien Ntaryamira ilidunguliwa katika anga la Kigali,Rwanda.Kulipuliwa kwa ndege hiyo ilikuwa kama ndio mwanzo wa mauaji makubwa ya kimbali "RWANDA GENOCIDE"

Kwa siku mia moja zaidi ya watutsi na wahutu wenye msimamo wa wastani kati ya  laki nane na milioni moja wanakadiriwa waliuawa.

4 July 1994, Paul Kagame na RPF wanafanikiwa kuwazidi  nguvu utawala wa kihutu ulioongozwa na Jean Kambanda na kurejesha hali ya utulivu.Wanamgambo waasi wa kutoka kabila la wahutu Ntarahamwe hatimaye wanakimbilia Congo.

Kwa kifupi huyo ndio mtu ambaye kwa baadhi yao ni shujaa ila kwa wengine ni kinyume chake.

Binafsi namtakia maisha mema na marefu katia kurejesha mahusiano zaidi kati wahutu na watutsi na kujenga Rwanda mpya.

Happy birthday Paul Kagame!

Thursday, October 22, 2009

Mtoto albino akatwa shingo

Picha ya watoto wenye ulemavu wa ngozi(Albino) wanaoishi kwa hofu kila kukicha ndani ya nchi yao.

Mwanafunzi wa darasa la pili,shule ya msingi Nyawilimilwa,Gasper Elikana(10) ameuwawa kikatili kwa kukatwa kichwa na kisha kunyofolewa mguu wake.Tukio hilo limetokea wilaya ya Geita,mkoani Mwanza.

 Pia wauaji hao walimjeruhi vibaya sana baba mzazi wa marehemu wakati akijitahisi kumwokoa mtoto wake na mauti.

Uko wapi ubinadamu wetu?Mateso haya na hofu kwa wenzetu mpaka lini?

Binafsi nalaani kwa nguvu zote na jeshi la polisi kwa kushirikiana na jamii kuhakikisha wahusika wanafikishwa mbele ya vyombo vya sheria.Hiyo pekee haitoshi,wahusika lazima wataje walipokuwa wanapeleka huo mguu.

Nawapo pole familia kwa kuondokewa na mtoto wao.Mwenyezi Mungu amwezeshe kupona haraka baba mzazi wa marehemu.

Mwenyezi Mungu wa rehema aipumzishe roho ya mtoto Gasper mahala pema peponi.Amina

Tutafika kweli kwa hali hii?