PICHA #1 Kikosi cha jeshi la wanamaji(Navy).Wakijitutumua kuonyesha ukakamavu siku ya dec 9 uwanja wa uhuru.Leo sijawaona Police Marine,Jeshi la majini (Navy) katika kurescue/kuongeza nguvu maana kikosi cha uokoaji cha jiji nacho KINAHITAJI KIOKOLEWA kwa mafunzo na VITENDEA KAZI..Nisaidieni hivi ni vikosi vya gwaride?Lazima serikali na wadau kutambua kuwa TAIFA LISILO JIANDAA KUKABILIANA NA MAJANGA NI TAIFA LINALOSUBIRIA MAAFA.
PICHA #2 Kwa kutumia vifaa walivyonavyo waokoaji wa
PICHA NAMBA 3 mbili .Nina hakika leo vikosi vya uokoaji vya jiji la dsm,navy,jeshi,polisi walikuwa na uwezo wa kuingia karibu kila kona kuhakikisha hakuna mtu aliyekwama kutokana na maji kujaa kila kona.Sio kwamba natoa LAWAMA ila NAKUMBUSHA kuna watu HAWAKO "SERUOIS"..
Picha na Ahmad Issa Michuzi
PICHA # 3 SWALI Hivi zile bilioni zaidi ya 60 tulizotumia siku chache zilizopita kwenye "
SIKUKUU YA UHURU"tungewekeza japo kununua vifaa vya uokoaji au unafikiri ni pesa zile ni ndogo.TANZANIA TATIZO SIO PESA..Jibu unaweza kuwa nalo hata wewe.
PICHA # 4 Kikosi cha uokoaji cha "wenzetu" wakiwa na vifaa na vitendea kazi vya kutosha walivyonunua kwa kutumia pesa za walipa kodi ili kuwawezesha kuingia mlango hadi mlango wakati wakisaidia kuokoa watu walikwama kwenye nyumba baada ya mafuriko kutokea.TANZANIA MIAKA 50 baada uhuru TUNAWEZA KABISA KUWA NA VIKOSI VYENYE VIFAA KWA AJILI KUPUNGUZA KAMA SI KUEPUSHA MAAFA ZAIDI WAKATI MAJANGA .SERIKALI PESA TUNAYO TATIZO MATUMIZI
PICHA # 5 Pichani askari wa kikosi cha "rescue" cha serikali ya Tanzania wakitumia "teknolojia yao" kutafuta waanga wa mafuriko.Kwa hali hii vikosi vya uokoaji vinahitaji kuokolewa pia na kupewa itendeakazi.Picha na
Ahmad Issa MichuziBinafsi natumia fursa hii kuwapa pole wote waliokubwa na janga hili.Tunaomba mwenyezi Mungu awatie nguvu ktk kipindi hiki kigumu.
Kwa watendaji pia wajipange zaidi jinsi ya kuwezesha vikosi vya uokoaji viwe na uwezo wa kukabiliana na majanga kwani uwezo wa kufanya hivyo tunao.Tunaambiwa mpaka sasa hakuna aliyefariki dunia.TUNAMSHUKURU MUNGU KWA HILO ila je vikosi vimeweza kuingia nyumba hadi nyumba na kujiridhisha hakuna mtu aliyenasa sehemu?Mungu aepushilie mbali.
Tuunganishe nguvu kwa pamoja ili kusaidia wenzetu waliopata na janga hili.
Tupo pamoja
Tufafika tu