Thursday, January 26, 2012

RAFAEL NADAL BEATS ROGER FEDERER (Australian Open Semi Final 2012

Raphael Nadali 25(Spain)

Kwa wapenzi wa Tennis.Rafal Nadal amemwaga bila huruma rafika na mpinzani wake Roger Federer (Swiss)

Mchezo ulikuwa wa kuvutia huku ukiwa wa piga nikupe.

Hongera Nadal..

Habari zaidi unaweza kuchungulia AUSTRALIAN OPEN

Friday, December 30, 2011

MWANAHABARI JOHNA NGAHYOMA AFARIKI DUNIA -RIP

Enzi za uhai wake mwandishi mkongwe marehemu John Ngahyoma(kushoto) akifanya mahojiano.

Mwanahabari mkongwe wa shirika la utangazaji BBC bw John Ngahyoma ameaga dunia leo asubuhi jiji Dar es salaam.

Enzi za uhai wake aliwahi kufanya kazi katika kituoa cha Radio Tanzania Dar es salaaam(RTD),ITV na baadaye TVT mpaka mauti yanamfika alikuwa BBC.

Msiba upo nyumbani kwa marehemu Tabata jirani na nyumba ya Danny Mwakiteleko.

Taarifa imetolewa na katibu mkuu jukwaa la wahariri BwNeville Meena.

Pole Glorie Ngahyoma pamoja na ndugu jamaa na marafiki.Mwenyezi Mungu awatie nguvu ktk kipindi hiki kigumu mnachopita.

Mwenyezi Mungu aile roho ya marehemu mahala pema peponi.AMINA

Thursday, December 29, 2011

BI HALIMA MCHUKA HATUNAYE TENA - R.I.P

Bi Halima Mchuka enzi za uhai wake.

Leo nimepokea habari ya kustusha baada ya kutembelea ukurasa wa Facebook wa mmoja wa marafiki zangu na kukutana na picha na habari mtangazaji mkongwe Bi Halima Mchuka hatunaye tena kaaga Dunia.

Kwa mujibu wa Mkurugenzi Mkuu wa TBC Clement Mshana, Bi HALIMA MCHUKA alikimbizwa katika hospitali ya DAR GROUP na baadae katika hospitali ya Taifa ya MUHIMBILI hapo jana baada ya kuanguka ghafla akiwa katika kituo chake cha kazi eneo la PUGU ROAD Jijini DSM.

Binafsi nilibahatika mara kadhaa miaka hiyo kumsikiliza akitangaza mpira wa miguu.Hakika alijaaliwa kipaji na alikuwa na mapenzi na soka.Bi Halima Mchuka atakumbukwa kwa historia aliyojiwekea ya kuwa mtangazaji wa kwanza mwanamke wa soka katika ukanda wetu wa afarika ya mashariki.

Mwenyezi ailaze roho ya Bi Halima Mchuka mahala pema peponi .Amina

Friday, December 23, 2011

Tanzania Broadcasting Corparation(TBC) WEBSITE-R.I.P

Bw Danstan Tido Mhando

MWAFRIKA wa kwanza kuongoza Idhaa ya Kiswahili ya Radio ya Shirika la Utangazaji la Uingereza (BBC), Danstan Tido Mhando,

Bw Tido Mhando baada ya kustaafu BBC Swahili akarejea nyumbani na kuwa mkurungezi mtendaji wa TBC(Tanzania Broadcasting Cooperation) kufanya MAPINDUZI makubwa.TENDA WEMA NENDA ZAKO,,mbali na yote hayo serikali iliamua kutomuongezea mkataba wa kazi na kumuweka pembeni.

Wachambuzi wa mambo ya habari wanaamini hayo yalifanyika kwa kile kilichoonekana serikali kutofurahia jinsi TBC iliyotoa fursa sawa kwa vyama vyote vya siasa wakati wa uchanguzi 2010.

Bw Tido Mhando kwa kuwa ni mtu anaye heshimika ktk tansia ya habari,kwa sasa habari za kuaminika amechukuliwa na Al jaazera swahili ambayo inatarajia kwenda hewani kuanzia 2012.
Popote alipoa aliondoka kama shujaa aliyetimiza wajibu wake.Hivyo ndivyo ninavyoamini.

Bw. Clement Senzota Mweta Mshana.

Bw.Clement Mshana alikuwa mkurugenzi wa Idara ya habari(MAELEZO).

April 21,20011 Rais Jakaya Kikwete alimteua Bw Mshana kuchukua nafasi ya Bw Tido Mhando kuwa mkurugenzi mtendaji wa shirika la utangazaji tanzania (TBC).

KAZI aliyofanya Bw Mshana ni KUHARIBU yale mazuri yaliachwa na kurejea YALEE YALEE KUHARIBU kama tulivyoweza kuharibu mashirika ya umma kama vila KAMATA ,UDA n.k

Leo naangalia habari kupitia TBC nakuta last update website ilikuwa november 5..ukitaka kuamini click www.tbc.co.tz

BW Mshana usilale,jifunze kutoka kwa majirani tusiende nchi za mbali.

RWANDA ( Rwanda Berau of Information and Broadcasting)
KENYA ( Kenya broadcasting corporation)
UGANDA ( Uganda broadcasting corporation)
TANZANI ( Tanzania broadcasting corporation) aibu aibu usipoteza muda kuclick


SWALI?
1.Hivi ni kweli hatuna watu wenye utalaamu wa kuupade website?Kama tunao tatizo nini?


2.Sasa TBC hiyo website ya kazi gani?tupo serious kweli?


Mungu ibariki Tanzania..

TUTAFIKA TU.






Wednesday, December 21, 2011

POLENI KWA MAFURIKO..TUMEJIANDA VIPI KUKABILIANA NA MAJANGA?

PICHA #1 Kikosi cha jeshi la wanamaji(Navy).Wakijitutumua kuonyesha ukakamavu siku ya dec 9 uwanja wa uhuru.Leo sijawaona Police Marine,Jeshi la majini (Navy) katika kurescue/kuongeza nguvu maana kikosi cha uokoaji cha jiji nacho KINAHITAJI KIOKOLEWA kwa mafunzo na VITENDEA KAZI..Nisaidieni hivi ni vikosi vya gwaride?Lazima serikali na wadau kutambua kuwa TAIFA LISILO JIANDAA KUKABILIANA NA MAJANGA NI TAIFA LINALOSUBIRIA MAAFA.
PICHA #2 Kwa kutumia vifaa walivyonavyo waokoaji wa PICHA NAMBA 3 mbili .Nina hakika leo vikosi vya uokoaji vya jiji la dsm,navy,jeshi,polisi walikuwa na uwezo wa kuingia karibu kila kona kuhakikisha hakuna mtu aliyekwama kutokana na maji kujaa kila kona.Sio kwamba natoa LAWAMA ila NAKUMBUSHA kuna watu HAWAKO "SERUOIS"..Picha na Ahmad Issa Michuzi


PICHA # 3 SWALI Hivi zile bilioni zaidi ya 60 tulizotumia siku chache zilizopita kwenye "SIKUKUU YA UHURU"tungewekeza japo kununua vifaa vya uokoaji au unafikiri ni pesa zile ni ndogo.TANZANIA TATIZO SIO PESA..Jibu unaweza kuwa nalo hata wewe.
PICHA # 4 Kikosi cha uokoaji cha "wenzetu" wakiwa na vifaa na vitendea kazi vya kutosha walivyonunua kwa kutumia pesa za walipa kodi ili kuwawezesha kuingia mlango hadi mlango wakati wakisaidia kuokoa watu walikwama kwenye nyumba baada ya mafuriko kutokea.TANZANIA MIAKA 50 baada uhuru TUNAWEZA KABISA KUWA NA VIKOSI VYENYE VIFAA KWA AJILI KUPUNGUZA KAMA SI KUEPUSHA MAAFA ZAIDI WAKATI MAJANGA .SERIKALI PESA TUNAYO TATIZO MATUMIZI

PICHA # 5 Pichani askari wa kikosi cha "rescue" cha serikali ya Tanzania wakitumia "teknolojia yao" kutafuta waanga wa mafuriko.Kwa hali hii vikosi vya uokoaji vinahitaji kuokolewa pia na kupewa itendeakazi.Picha na Ahmad Issa Michuzi

Binafsi natumia fursa hii kuwapa pole wote waliokubwa na janga hili.Tunaomba mwenyezi Mungu awatie nguvu ktk kipindi hiki kigumu.

Kwa watendaji pia wajipange zaidi jinsi ya kuwezesha vikosi vya uokoaji viwe na uwezo wa kukabiliana na majanga kwani uwezo wa kufanya hivyo tunao.Tunaambiwa mpaka sasa hakuna aliyefariki dunia.TUNAMSHUKURU MUNGU KWA HILO ila je vikosi vimeweza kuingia nyumba hadi nyumba na kujiridhisha hakuna mtu aliyenasa sehemu?Mungu aepushilie mbali.

Tuunganishe nguvu kwa pamoja ili kusaidia wenzetu waliopata na janga hili.

Tupo pamoja

Tufafika tu

Wednesday, December 14, 2011

Wabunge wana HAKI ya kupewa pia SLEEPING ALLOWANCE

Wananchi wa jimbo la Mbinga wakitaabika na barabara mbovu.

Mh John Komba mbunge wa mbinga(CCM) akicha usingizi ikiwa ni njia mmoja wapo inayotumiwa na wabunge kuwakilisha wananchi.


Mtazame mh anavyouchapa usingizi wakati wapiga kura wake wanataabika na matatizo kibao.

Nashauri kwa wale wabunge wasaliti wanaopigania kupewa posho za vikao sitting allowance laki mbili kwa siku wasisahau kuomba pia Sleeping allowance maana wengine wanapiga tu usingizi.

Tutafika tu

Friday, December 9, 2011

Hongera Tanzania miaka 5O uhuru..Changamoto bado nyingi.

Mtanzania akiwa amebebwa na "ambulance" akipelekwa kupata tiba(iwapo itapatikana) miaka 50 baada ya uhuru.

Taifa changa duniani Sudani kusini ambalo halijasherekea hata mwaka mmoja wakitumia NJIA mbalimbali ili kuhakikisha wananchi wake wanapata huduma ya afya hadi vijijini..Tunajifunza nini?

Leo nchi yangu imetimiza miaka 50.

Hongera sana kwa watanzania wote popote walipo.Kuna "mengi ya kupongezwa" kwa hapa tulipo lakini naamini hata WAO wanajua tunamengi yalio ndani ya uwezo wetu jamii au viongozi hawajitimiza wajibu wao mpaka kupelekea hapa tulipo.

Chukulia mfano hizo picha hapo juu.Tunao mabwana afya hadi ngaji ya kijiji lakini unamkuta hana vitendea kazi mfano hata jinsi ya kumfikia mwananchi.Lazima wadau wote,serikali,mtu mmoja mmoja tusimame kwa sauti na vitendo kuhakisha tunasherekea kwa sababu za msingi.

Bado tunasafari ndefu tulistahili kuwa mbali zaidi ya hapa.Na tunastahili kuwa mbali zaidi ya hapa.

Hongera Tanzania ingawa badi unachamoto nyingi..Rushwa,miiko ya maadili/utawala bora matumizi mazuri ya raslimali na kodi za watanzania.

Tutafika tu