Monday, April 23, 2012

Rais wa Zanzibar aongoza mazishi ya Brigedia Jenerali Mwakanjuki

Rais Jakaya Kikwete akitoa heshima za mwisho kwa marehemu Brigedia Jenerali Adam Mwakajuki muda mfupi kabla ya kusafirishwa kwenda Zanzibar kwa mazishi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohammed Shein akiweka udongo kaburini.

Rais mstaafu wa Zanzibar mh Amani Abeid Karume akiweka udongo kaburini.
Familia ya marehemu Brigedia Jenarali wakiweka shada la maua .
Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Balozi Seif Ali Iddi(kushoto), akijumuika na Waumini wa madhehebu ya Anglikana Mkunazini katika Ibada ya kuuombea mwili wa Marehemu Brigedia Mwakanjuni, aliyefarika april 19 Mjini Dar-es- Salaam.
Mtoto wa Marehemu Bw Aliko Mwakanjuki akiwa na Msalaba wakati wakitoka Kanisani baada ya ibada ya kumuombea marehemu Brigedia Adam Mwakanjuki.
Mke wa Brigedia Mstaafu Adam Mwakanjuki Mama Ikupa Adam Mwakanjuki (kushoto) pamoja na Agness Mwakanjuki(kulia) wakishiriki ibada ya kumwombea marehemu.
Watoto wa marehemu Che Mwakanjuki akifuatiwa na Aliko Mwakanjuki wakiweka udongo kwenye kaburi la baba yao.
Askofu Mstaafu John Ramadhani, akiongoza ibada ya mazishi katika makaburi ya Mwanakwerekwe.
Mchungaji Majaliwa wakati wa Ibada ya Kumuombea marehemu Brigedia Mstaafu Adam Mwakanjuki.


Jumapili april 22,2012 Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk.Ali Mohammed Shein,ameongoza maelfu ya wananchi na viongozi mbali mbali wa Serikali katika mazishi ya aliyekuwa Brigedia Jenerali Msataafu Marehemu Adam Clement Mwakanjuki ambayo yamefanyika Makaburi ya Mwanakwerekwe Zanzibar.

Mazishi hayo ambayo yalifanyika kwa heshima zote za kijeshi kwa kupigwa mizinginga 11 baridi, yalihudhuriwa pia na Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzani Dk.Gharib Bilal,Rais Msaafu wa Zanzibar Aman Abeid Karume,na viongozi wengine wa ngazi za juu wa Vyama vya siasa na Serikali.

Chanzo:Asante Othuman Mapara kwa picha

Blog hii inawapa pole familia kwa msiba huu.Mwenyezi Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu.Pumzika kwa amani Brigedia Generali Adam Mwakanjuki.Amen




No comments: