Sunday, October 26, 2008

DADA MTANZANIA AJITOSA UDIWANI FINLAND

Wakazi wa jiji la tampere wakicheki picha za wagombea.




Picha ya Dada Emma Palonen ya nne kutoka kulia mstari wa chini




Sehemu ya Tangazo la likionyesha namba 107 ambayo ndio ya Emma


Dada Emma Palonen ni mtanzania mbaye anaishi hapa Tampere.Nimekuta leo picha yake kwenye bango akiwa ni mmoja wa wagombea udiwani katika manispaa ya Tampere.


Binafsi nilifarijika kwanza,namfahamu binafsi kama ni dada mchapakazi,anajiamini na anauwezo mzuri wa kujenga hoja.


Nilipo ona picha yake kwenye bango nilitaka kumtafuta kupata 'mawili matatu' kuhusu yenye kwenye ulingo wa siasa lakini muda ukawa haruhusu.Ila nitamtafuta na kuwaletea mahojiano naye.


Dada Emma anagombea nafasi ya udiwani kupitia Chama cha Christian Democrats.

Kwa mfumo wa hapa unachagua namba ya mgombea umtakaye.

Hivyo kwa wakazi wa Tampere wenye sifa za kupiga kura unaweza kusoma kwa kubofya HAPA.

Tujitokeze kesho tarehe 26 october,2008 chagua number 107



Kila la kheri dada Emma nakuombea ufanikiwe katika uchaguzi.Tupo pamoja.



Umeanzisha Safari..naamini ..TUTAFIKA TU.




11 comments:

Anonymous said...

ni habari njema sana ..

ndio maana nawaambia wanakina dada wenzangu tunaweza mambo mengii sio tukalie tu kusubiria kila kitu cha upendeleo
.
Hongeera dada Emmma


safi edo naona siku hizi umeikumbuka blog yako baab kubwa

Jane,spain

Anonymous said...

Tatizo wakinadada au wanawake wengi hivi kwanini hatupendani?Maana usishangae hapo finland unaweza kuna wakinadada kibao wenye sifa za kupigakura ila kwa wivu utakuta watamnyima mwanamke mwenzetu na kuwapa hao wakina mc cain wa finland

MKOKOZI MWANZA said...

Hongera kila la kheri.

Ningekuwa huko hakika kura yangu ingekuwa yako.


Masai vipi mbona wewe ukugombea?aaaa aaaa

salam kwa wote huko kamanda

Anonymous said...

Vipi mbona ujatuwekea picha za FFU finland wakitoa ulinzi kwenye kampeni za huku?

si unajua huku kwetu uchaguzi lazima FFU ..mabomu ya machozi..

Anonymous said...

Anony ...October 26, 2008 3:15 AM

umenichekesha sana ...
ila kweli vipi huko kama Chadema na CCM wanatumia Chopa..helkopta vipi huko wanatumia KLM nini?

HOJA, SAUT

Anonymous said...

Huyo dada kaenda kuweka tu CV lakini wazungu walivyo wabaguzi tena nchi zenu hizo ambazo hazina hata askari mweusi..msahau ..

ila poa bora ajaribu

Anonymous said...

Emma all the best my sister..

utashinda..nimependa sana ulivyoamua kujiamini.

Yasinta Ngonyani said...

nami pia nasema hongera sana dada Emma. huko ndio kujiamini

Anonymous said...

hongera Dada stand there u are nakupongeza kwa hilo.

Edo siku hizi umekuwa na spid sana nakupongeza kwa hilo!kaza buti tupe mambo mazuri!

EDWIN NDAKI (EDO) said...

Asante sana Matty najaribu kasafari asante sana kwa kunitembelea na wenghine wote mnaotembelea ila muda haujatosha kwenu kuacha maoni..

nawapenda wote..asanteni

Kibunango said...

Vp Matokeo ya huyo mdada?